Saturday, March 16, 2024
WANANCHI MANISPAA YA SINGIDA WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO ZOEZI LA UHAKIKI...
Wednesday, March 13, 2024
Tuesday, March 12, 2024
RC DENDEGO APOKELEWA KWA KISHINDO MKOANI SINGIDA NA KUKADHIWA RASMI OFISI
Mkuu mpya wa Mkoa wa Singida
Halima Dendego, ameahidi kusimamia shughuli za maendeleo kwa niaba ya Rais Dk.
Samia Suluhu Hassan, na kutoa tahadhari kwamba kwenye uongozi wake hataki
kusikia suala la msamiati wa changamoto kama sababu mojawapo ya kukwamisha
maendeleo.
Dendego amesema hayo muda
mfupi alipokabidhiwa ofisi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo Peter Serukamba, na
kuzungumza na Watumishi wa ofisi hiyo, Kamati ya Ulinzi na Usalama, Viongozi wa
vyama vya siasa, Viongozi wa Dini na wageni waalikwa mbalimbali.
"Nimekuja Singida kupokea
majukumu ya kazi niliyopewa na Mheshimiwa Rais wa Hamguri ya Muungano wa
Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan, kama alivyoacha kaka yangu Serukamba, na mimi
nitasimamia ili tupige hatua mbele zaidi, nawahakikiahi kama aliyeondoka ni
Kulwa, basi aliyekuja ni Doto...lazima kazi ziendelee kwa ajili ya kuleta
maendeleo." alisema Dendego.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amesema ni lazima kazi zifanyike na majibu yapatikane katika utumishi wake huku akaisisitiza kuwa atakuwa msikivu mnyenyekevu na mtulivu kwa anaowaongoza na kusimamia shughuli na miradi ya maendeleo mkoani Singida.
Amewahakikishia utumishi
uliotukuka na ushirikiano wa dhati watumishi wote wa Mkoa wakiwemo wakuu wa
Wilaya za Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri ili kuwaletea maendeleo ya dhati
wananchi na Watanzania kwa ujumla wa Mkoa wa Singida.
Akizungumza kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Singida, Katibu Mwenezi wa chama hicho pamoja na kuwapongeza wakuu hao wa mikoa, alisema CCM itaendeleza ushirikiano wa dhati na Serikali ya Mkoa kwa lengo la kuwaletea wananchi maendeleo.
Awali aliyekuwa Mkuu wa Mkoa
aliyehamishiwa mkoani Iringa, Peter Serukamba, alitumia fursa hiyo kuzishukuru
kada mbalimbali za uongozi tangu awasili mkoani Singida mwaka mmoja na miezi
saba iliyopita na kufafanua kuwa amejifunza mengi ya maendeleo akiwa Singida.
Serukamba alisema akiwa
Singida anajivunia kupandisha matumizi ya mbolea ikilinganishwa na hali
aliyoikuta huku pia akifanikisha upatikanaji wa mbegu ya ruzuku kwa zao la
alizeti.
Serukamba alisema pia katika
kipindi chake mkoani Singida anajivunia kumaliza tatizo la mauaji lililokuwa
linaikabili Wilaya ya Manyoni kutokana na kukithiri kwa mauaji nyakati za usiku
na ufukuaji wa makaburi kutokana na imani za kishirikina.
Amesema kwa nguvu hiyo hiyo,
ndiyo atakayoenda nayo Iringa, kwa lengo la kupambana na kuongeza juhudi ili asiyashushe
maendeleo ya mkoa huo yaliyochagizwa na Mkuu wa Mkoa Halima Dendego,
aliyehamishiwa sasa mkoani Singida.
Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Singida, Katibu mwenezi wa CCM, Elphas Lwanji amesema kuwa, chama hicho kinaahidi kushirikiana na Serikali ya Mkoa huo kupitia uongozi wa Halima Dendego, kama ambavyo walimpatia Peter Serukamba.
Mkuu mpya wa Mkoa wa Singida Halima Dendego, akizungumza na viongozi na baadhi ya wananchi walioshiriki katika hafla ya makabidhiano ya ofisi yalifofanyika leo Machi 12, 2024 mkoani Singida.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa Peter Serukamba, akimkabidhi taarifa ya Mkoa wa Singida kwa Mkuu wa Mkoa huo Halima Dendego, wakati wa hafla ya makabidhiano ya ofisi.
Wakuu wa Mikoa wakiweka saini katika vitabu vya makabidhiano ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa Singida Machi 12, 2024
Saturday, March 09, 2024
SERUKAMBA AWAAGA WATENDAJI MKOANI SINGIDA KWA KUWAAGIZA MIRADI YOTE KUKAMILIKA KWA WAKATI
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter
Serukamba, leo tarehe 9 Machi, 2024 amehamishiwa kutoka Mkoa wa Singida kwenda
kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringia na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Halima Omar
Dendego, kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Singida huku akiwaagiza watendaji
kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati.
Kwa muujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 09 Machi, 2024 na Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses M. Kusiluka ambaye ni Katibu Mkuu Kiongozi, ikieleza mabadiliko madogo ya Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na wakurugenzi wa Halmashauri imeeleza kuwa uteuzi na uhamisho huo unaanza leo tarehe 09 Machi, na uapisho wa Wakuu wa Mikoa utapangwa baadaye.
Akiwa katika kikao cha kamati ya ushauri wa Mkoa (RCC) kilichofanyika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Singida Serukamba, ghafla alionyesha tabasabu na shahuku ya kuongea jambo huku wajumbe nao wakionesha tabasabu kwa kile kilichokuwa kimesambaa kwenye mitandao ya kijamii kikihusisha uteuzi na uhamisho huo.
Mara baada ya muda mfupi ndipo Serukamba aliposhindwa kuvumilia na kuamua kuwaambia wajumbe wa kikao hicho kwamba amehamishwa kutoka Mkoa wa Singida na kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa Halima Omar Dendego, kuhamia Mkoa wa Singida.
Aidha, Serukamba, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kumuamini katika nafasi hiyo na amemuahidi kuendelea kufanya kazi kwa bidii katika kuhakikisha anawatumikia Wananchi hao wa Mkoa wa Singida kikamilifu.
Hata hivyo Serukamba, amewashukuru Watumishi wa Umma wa Mkoa wa Singida, akianzia na Katibu Tawala Mkoa huo Dkt. Fatuma Mganga kwa ushirikiano aliyokuwa akiupata, watumishi wote wa Sekretarieti ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Makatibu Tawala wa Wilaya, Wakurugenzi, Viongozi wa Dini pamoja na Wananchi wote kwa ujumla.
Katika hatua nyingine, wajumbe wa kikao hicho wamempongeza aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo kwa katika kipindi chote cha uongozi wake Mkoani hapo wakisema hakika amekuwa ni kiongozi aliyekuwa akisukuma maendeleo ya mtu mmoja mmoja na wanasingida kwa ujumla hasa katika suala la kilimo cha utumiaji mbolea.